Swahili
Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya count 26
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ
( 1 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 1 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 1](style/islamic/icons/mp3.png)
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ
( 2 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 2 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 2](style/islamic/icons/mp3.png)
Siku hiyo nyuso zitainama,
عَامِلَةٌ نَّاصِبَةٌ
( 3 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 3 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 3](style/islamic/icons/mp3.png)
Zikifanya kazi, nazo taabani.
تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً
( 4 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 4 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 4](style/islamic/icons/mp3.png)
Ziingie katika Moto unao waka -
تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ
( 5 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 5 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 5](style/islamic/icons/mp3.png)
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍ
( 6 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 6 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 6](style/islamic/icons/mp3.png)
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِن جُوعٍ
( 7 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 7 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 7](style/islamic/icons/mp3.png)
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاعِمَةٌ
( 8 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 8 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 8](style/islamic/icons/mp3.png)
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ
( 9 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 9 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 9](style/islamic/icons/mp3.png)
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ
( 10 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 10 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 10](style/islamic/icons/mp3.png)
Katika Bustani ya juu.
لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً
( 11 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 11 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 11](style/islamic/icons/mp3.png)
Hawatasikia humo upuuzi.
فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ
( 12 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 12 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 12](style/islamic/icons/mp3.png)
Humo imo chemchem inayo miminika.
فِيهَا سُرُرٌ مَّرْفُوعَةٌ
( 13 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 13 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 13](style/islamic/icons/mp3.png)
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
وَأَكْوَابٌ مَّوْضُوعَةٌ
( 14 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 14 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 14](style/islamic/icons/mp3.png)
Na bilauri zilizo pangwa,
وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ
( 15 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 15 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 15](style/islamic/icons/mp3.png)
Na matakia safu safu,
وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ
( 16 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 16 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 16](style/islamic/icons/mp3.png)
Na mazulia yaliyo tandikwa.
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ
( 17 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 17 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 17](style/islamic/icons/mp3.png)
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ
( 18 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 18 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 18](style/islamic/icons/mp3.png)
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ
( 19 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 19 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 19](style/islamic/icons/mp3.png)
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ
( 20 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 20 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 20](style/islamic/icons/mp3.png)
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنتَ مُذَكِّرٌ
( 21 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 21 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 21](style/islamic/icons/mp3.png)
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ
( 22 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 22 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 22](style/islamic/icons/mp3.png)
Wewe si mwenye kuwatawalia.
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
( 23 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 23 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 23](style/islamic/icons/mp3.png)
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ
( 24 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 24 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 24](style/islamic/icons/mp3.png)
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ
( 25 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 25 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 25](style/islamic/icons/mp3.png)
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم
( 26 ) ![Swahili - Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 26 Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya 26](style/islamic/icons/mp3.png)
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!